Thursday 23 November 2017

Habari wapenzi wa blog hii samahanini xana kwa kuwa kimya kwa muda kutokana na yaliyokuwa nje ya uwezo wetu kuyamudu ila tunawakaribisha tena upya ahsanteni

Thursday 28 April 2016

Mambo 10 yanaweza kuwa kama kichocheo cha usaliti katika ndoa ambayo hasa ni tatizo la moyo


Mambo 10 yanaweza kuwa kama kichocheo cha usaliti katika ndoa ambayo hasa ni tatizo la moyo

1. Kutokuvutia tena • Moja ya sababu iliyopelekea kukubali kuoa au kuolewa na huyo mwenzi wako, kuna baadhi ya vitu ulivutiwa navyo ndio akawaacha woote na kumchagua huyo. • Vitu hivyo usipovizingatia na kuvi “maintain” vitasababisha hali ya kukinai kwa mwenzi wako na mwisho kuanza kuvutiwa na wengine kule nje.
 
2. Kutokujali tena kuwa unaongezeka unene, kubadilika unavyoonekana na • Kila mwanandoa ana “test” yake ya mvuto kwa mwenzi wake. • Kuna mwingine alikupenda kwasababu ya wembamba wako sasa unapojiachia na kuwa mnene ila hamu ya kuendelea kuvutiwa nawe inapungua na baadaye inakwisha na kusababisha aanze kuchungulia nje ya “fance” • Kuna mwingine alikupenda kwasababu ya unene au kujazia katika maeneo Fulani Fulani. Sasa mwili ukiporomoka unapoteza ule mvuto tena na kumfanya apoteze hamu ya kuwa na wewe na kumfanya kuanza kuchungulia chungulia nje. • Ni vizuri kujali afya yako na kujua ni vitu gani vinavyomvutia mwenzi wako kutoka kwenye mwili wako na ujitahiti kuvitunza “maintain” ili kuendelea kudumisha ule mvuto kwa mwenzi wako. • Kumbuka kwamba tunaishi katika mwili. …
 
 
3. Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa. • Tendo la ndoa ndio mhimili unaoishikilia ndoa. • Ukiona hamu ya tendo la ndoa imepungua kwa mwenzi wako ujue majanga yanakunyemelea. • Kufanya tendo la ndoa mara chache miongoni mwa wanandoa ni ufa wa kubomoa ukuta na ulinzi wa ndoa. • Muda si mrefu utaanza kutamani wengine na mwisho wake utaangukia huko.
 
 
4. Kukosa hamu katika mavazi mazuri kwa ujumla, mtindo wa nywele na jinsi unavyoonekana. • Hili hasa ni kwa wanawake. Kable ya kuolewa ulikuwa unajitahidi sana kujipamba na kujitunza kila wakati ulikuwa safi na nadhifu. • Pochi yako ilikuwa haikosi vi pafyumu pafyumu. Sasa umesahau hata bei za pafyumu zinauzwaje. • Sasa umeolewa, unashinda na upande wa kanga au kitenge kifuani toka asubuhi mpaka jioni wala huna habari. • Mumeo kila akikuangalia mpaka haamini kama ni wewe aliyekuoa ukiwa mrembo na wa kuvutia. • Unavaa nguo nzuri tu pale tu unapotoka kwenda kanisani au mtoko maalumu.
 
5. Kukosekana kwa mawasiliano • Mawasiliano yanaushisha pande zote mbili. • Anayetoa na anayepokea
 
 
6. Kushindwa kuendeleza yale yanayompendeza kila mmoja wenu. • Mnakubaliana mipango kama wanandoa lakini utakelezaji unakua mgumu. • Mmoja anakuwa tayari kutekeleza na mwingine anashindwa. • Aliyetayari kutekeleza anavunjwa moya sana na Yule ambaye sio mtekelezaji
 
7. Ndoa za kipindi cha likizo. • Wanandoa wanaonana siku kumi na nne tu kasha kila mtu anasafiri kurudi anakofanya kazi. • Wapo baadhi ya wanandoa kutokana na mazingira yao ya kazi wanaonana kila baada ya miezi 6 au wengine hata mara moja kwa mwaka. • Hii hasa ni kwa wanandoa wanaofanya kazi mikoa mbali mabili au nchi mbalimbali. • Wanatafuta pesa wakiua ndoa zao kwajili ya kusaka pesa. • Ni heri kuacha kazi hiyo na kuishi maisha ya kawaida kuliko kuwa na ndoa kama hii. • Kiufupi hii sio ndoa. 
 
8. Kushindwa kushirikiana chumba cha kulala. • Zipo baadhi ya ndoa mume analala chumba chake na mke analala chumba chake. • Wapo wanandoa pia ambao wanalala chumba kimoja ila vitanda tofauti • Kuna wengine wanalala chumba kimoja ila mmoja analala kitandani na mwingine analala chini.

9. Kushindwa kumfikisha mwenza wako mara kwa mara katika tendo la ndoa. • Sio swala la kushiriki tu. • Mnaweza mkawa mnashiriki lakini je ushirika huo unamridhisha kila mmoja wenu? • Mmoja anapokuwa anapunjika kila siku anakula lakini hashibi, inafungua mlango wa kumtafuta mshibishaji mwingine ili aweze kumshibisha. • Tatizo hili ni kubwa sana hasa kwa siku za leo. • Wanaume wengi ni wavivu na wenye ubinafsi. • Wanalishwa vizuri ila wanajishibisha wenyewe tu na kuwaacha wake zao wakiishi kwa njaa ya muda mrefu na matokeo yake michepuko imekuwa ikiongezeka kila iitwapo leo.
 
 
10. Kufanya kazi pamoja mwanamke na mwaname asiye mwenzi wako kwa muda mrefu. • Sumaku na bati vikikaa karibu mwishowe vitanasa. • Mwanamke na mwanaume wanaofanya kazi pamoja kwa muda mrefu wakiwa katika mazingira ya private huishia katika kutamaniana. • Kazi za kusafiri kwa pamoja mwanamke na mwanaume na kukaa hotel moja kikazi wakiwa wawili tu huweza kuongeza kazi ya ziada ambayo ni sumu kwa ndoa zao. • Kwenda kusoma pamoja kozi za nje kati ya wawili hao, wanaweza kuvumila sikuchache za kwanza na baada ya hapo huweza kujikuta wakiwa katika ukurasa mwingine. • Kwenda safari mbali za kikazi pamoja umakini usipozingatiwa ni majanga. • Kufanya vikao katika vyumba vya hotel mwanamke na mwanaume. • Kujifungia kufanya counselling au maombezi mwanamke na mwanaume wawili tu chumbani ni majanga. • Kujifungia chumbani mwanaume na mwanamke wawili tu kusoma na kubukua kwajili ya mtihani ni majanga

MMEGOMBANA? FUATA MBINU HIZI KURUDISHA MAPENZI


Kugombana ni jambo ambalo halikwepeki katika uhusiano wa kimapenzi. Upo ugomvi ambao ni wa kawaida na huisha kirahisi lakini upo ugomvi ambao huwa mkubwa na kama ukitokea na ukashindwa kujua nini cha kufanya kuweka mambo sawa, husababisha ufa kwenye penzi lenu.Leo tutazungumzia mambo muhimu ya kufanya inapotokea wewe na mpenzi wako mmeingia katika ugomvi mkubwa, mmetoleana maneno machafu au hata kupigana.

1. TAFAKARI CHANZO CHA TATIZO
Kuna usemi kwamba ukitaka kulitatua vizuri tatizo ni lazima kwanza ujue chanzo cha tatizo lenyewe. Ukishindwa kugundua chanzo cha tatizo, basi na wewe unakuwa sehemu ya tatizo.
Utashangaa kwamba wapenzi wengi hugombana na mambo kuwa makubwa kabisa kwa sababu ya vyanzo vidogo ambavyo walishindwa kuvigundua mapema na matokeo yake vikazaa matatizo mengine.
Mfano rahisi, chanzo kinaweza kuwa mpenzi wako amekupigia simu lakini ukashindwa kuipokea kwa muda muafaka. Atakapopiga kwa mara nyingine au mkikutana, usitegemee atakufurahia kwa sababu atahisi umemdharau kwa kutopokea simu yake.Endapo ukifanya makosa ya kushindwa kuliona kosa lako mapema na kushindwa kuomba radhi au kutoa maelezo yanayoeleweka kwa nini hukupokea simu, matokeo yake utamjibu vibaya, naye atakujibu vibaya na mwisho mtaishia kupigana au kuachana kabisa mkiwa mmeshatoka kabisa kwenye kosa la msingi.
Bila shaka msomaji wangu umeona jinsi chanzo kidogo kinavyoweza kusababisha tatizo kuwa kubwa. Ndoa nyingi au uhusiano unaofika mwisho huwa umesababishwa na mambo madogo ambayo yalishindwa kutafutiwa suluhu mapema.
Katika kila ugomvi unaotokea, jambo la kwanza jipe muda wa kutafakari chanzo kilichosababisha mkagombana. Wakati mwingine wewe ndiyo unaweza kuwa chanzo cha tatizo lakini kama ukiyajua makosa yako mapema na kukiri kisha kuomba radhi kwa mwenzio, utakuwa kwenye nafasi nzuri ya kurudisha mapenzi kwa haraka.

2. MPE MUDA HASIRA ZIISHE
Kila binadamu ameumbwa akiwa na hasira na kwa bahati mbaya ni wachache wanaoweza kuzidhibiti hasira zao. Ni rahisi mtu kutukana, kupiga au kuharibu vitu akiwa na hasira.Baada ya kugombana, kila mmoja lazima atakuwa na hasira na njia pekee inayoweza kuepusha matatizo zaidi, ni kujipa muda na kumpa muda mwenzako ili hasira zipungue.
Kama mpo sebuleni na umetokea ugomvi, ni busara kwenda chumbani au nje mpaka hasira zako zikiisha. Ni makosa kulazimisha suluhu wakati kila mmoja akiwa na jazba kwani mtaishia pabaya zaidi.
Ukishaona hasira zako zimetulia na mwenzako naye ametulia, unaweza kuanzisha mada juu ya kilichosababisha mkagombana. Tumia lugha ya upole kwani endapo utakuwa ukifoka au kuzungumza kwa sauti ya juu, matokeo yake mtarudia tena kugombana.

3. MPE NAFASI YA KUZUNGUMZA
Huwezi kumuelewa mtu kabla hujampa nafasi ya kuzungumza na kumaliza kile alichokusudia kukisema. Endapo tatizo limetokea na upo kwenye hatua za kusaka suluhu, mpe mwenzako nafasi ya kueleza dukuduku lililopo ndani ya moyo wake.
Usimkatishe wala kumbishia chochote, muache aongee ulichomuudhi mpaka dukuduku lake liishe kisha na wewe jieleze kwa upole na sauti tulivu.

4. OMBA MSAMAHA
Hakuna silaha nzuri inayoweza kukusaidia kuushinda ugomvi wowote na kutuliza mambo kabla hayajawa mabaya kama kuomba msamaha. Neno ‘samahani’ ni dogo lakini lina maana kubwa kwa yule mtu anayelitoa na anayelipokea.
Hata kama unaona dhahiri kwamba kosa siyo lako, omba msamaha kwanza kisha baada ya hapo anza kumuelewesha mpenzi wako kwa upole. Lazima mwisho na yeye atayaona makosa yake na kukuomba msamaha, mtaweza kuepuka kuukuza ugomvi huo na kurudisha hisia za mapenzi.


5. USIWEKE KINYONGO
Endapo umeamua kuomba msamaha kwa mpenzi wako, au yeye amekuomba msamaha, samehe kwa dhati kutoka ndani ya moyo wako na sahau kile kilichotokea. Ni kosa kubwa kuweka kinyongo rohoni, yaani unamwambia kwamba umemsamehe wakati moyo wako bado una hasira naye. Ukisamehe kwa dhati, jifunze na kusahau kwani kusamehe kunaenda sambamba na kusahau.
Wazungu wanasema forgive and forget. Elewa kwamba mpenzi wako ni binadamu ambaye hajakamilika, wala si malaika.
Lazima atakuwa akikosea mara kwa mara, endapo utakuwa ukilimbikiza vinyongo, unafuga matatizo makubwa kwani siku nyingine akikukosea hata jambo dogo, utakumbushia na ya jana na juzi na mwisho ugomvi utakuwa mkubwa sana.
Kwa maoni, ushauri au swali nicheki kwa namba za hapo juu

NI NINI MAANA YA MAPENZI!


NI NINI MAANA YAMAPENZI!


Katika kuongelea suala zima la mapenzi ni vigumu kujua maana halisi ya mapenzi kwa maana halisi ya mapenzi ni kutokana na mtu mwenyewe anavyoona.
Lakini kwa ujumla mapenzi ni ile hali ambayo watu wawili wanaingia katika mahusiano ambayo yanabeba mambo mengi iliwemo uvumilivu,kuchukuliana katika mambo yote yanayo husu maisha kwa ujumla.

MSINGI HASA WA MAPENZI 

      1-UVUMILIVU
2-HEKIMA
3-BUSARA
4-UPENDO
5-UWAZI
    6-HESHIMA

1-Uvumilivu katika mapenzi ni suala la msingi sana kwani kama nilivyotangulia kusema kuwa mapenzi ni kama safari ambayo ina mambo mengi ikiwemo mateso na mabadiko mbali mbali. kwa hiyo bila uvumilivu ni kazi bure.
2-Hekima ni hali ya kunyenyekea. ili mapenzi yaweze kuwa mapenzi lazima kuwe na unyenyekevu wa kutosha.
3 Busara ni hali ya kutengeneza uelewano na kuondoa tofauti eitha ya ki maneno au matendo.
4 Upendo ni hali ya kutengenza imani imara na sawia baina yenu wawili.
5 Uwazi ni hali ya kusomana na kufamiana ki myoyo kimwili na kifikra baina ya watu hawa wawili.
6 Heshima nayo pia ni njia kuu ya kuengeneza maelewano sawiya.

Saturday 23 April 2016

VIGEZO 10 VYA KUMPATA MUME/MKE /MCHUMBA MWENYE MAPENZI YA KWELI


          VIGEZO 10 VYA KUMPATA   MUME/MKE /MCHUMBA MWENYE      MAPENZI YA KWELI


Wengi wamejikuta wakiitwa wahuni kutokana na kuwa na uhusiano wa kimapenzi na makundi ya wanaume au wanawake. Hata hivyo wachunguzi wa masuala ya mapenzi wanasema idadi kubwa ya wapenzi si kigezo sahihi cha kupima tabia ya mtu na kumhusisha na uhuni.
Watalaam hao wanataja safari ya kupata chaguo halisi la mwanaume/mwanamke wa maisha ndiyo inayowaponza wengi kiasi cha kujikuta wameingia katika kashfa ya kuwa na uhusiano na dazeni ya wapenzi.

Wanasema msichana/mvulana anayeingia katika uwanja wa mapenzi kwa kuwa na hisia za kufanya ngono, hukosa umakini wa nani anafaa kuwa mpenzi wake kutokana na kukosa elimu ya uhusiano kutoka kwa wazazi wake.

Kwa mantiki hiyo, bila upembuzi wa kina, mtu asiye na elimu ya jinsi ya kumpata mpenzi wa kweli hujikuta ameangukia kwa mwanaume/mwanamke asiyemfaa, ambapo baadaye huamua kuachana na huyo na kwenda kwa mwingine kujaribu bahati tena ya kupata penzi la kweli.

Zinatajwa zawadi, hitaji la kusaidiwa kimaisha, mvuto wa kimahaba na mazoea kuwa ni vichocheo vinavyowaangusha wengi kwenye mapenzi na wasiowafaa.

Ukweli ni kwamba mtu aliyenaswa kwa ‘ujinga’, huwa hakatwi kiu ya penzi na mwanaume/mwanamke asiye chaguo sahihi la maisha yake. Hivyo hufikia maamuzi ya kujiingiza katika uhusiano mpya mara 2,3,4,5 na kujikuta wakiambulia wanaume/wanawake wale wale wasio sahihi kwake.

Mwanamnke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Ramla aliwahi kuniomba ushauri, akasema amechoka kuchezewa, maana kila mwanaume anayempata anakuwa si chaguo lake. Lakini kibaya zaidi kuachia ngazi au kutemwa huku akiwa tayari ameshafanya mapenzi na wanaume hao.

Na leo my best friend na mdau wangu mkubwa wa Blog hii  Rayha ametaka kujua vigezo gani vya kuzingatia ili kumpata mume/mpenzi borana mwenye mapenzi ya kweli na ya dhati , hii ameiandika kwenye ukurasa wake wa facebook.

Nia ya swali lake ilikuwa ni kuniomba njia za kumtambua mwanaume mkweli bila kufanya naye mapenzi? Aliuliza hivyo huku akiwa na hoja kuwa wanaume wengi hawako tayari kuwa na uhusiano na msichana bila kufanya naye mapenzi na wakati huo huo huficha tabia zao chafu wakilenga kumnasa wamtakaye.

Binafsi nafahamu kuwa kuna wanawake/wanawake wengi ambao hujiingiza katika mapenzi kwa kutekwa na hadaa za mwili na kujikuta wanacheza mchezo wa kitoto wa pata potea.

 Ni madhumuni ya somo hili kufundisha vigezo vya kumpata mwanaume/mwanamke halisi wa maisha, bila kufanya naye mapenzi. Njia hii ina faida kwa pande zote mbili yaani kwa mwanamke na mwanaume kwani kuacha au kuachwa bila kufanya mapenzi ni bora kuliko kuwa muonjaji, tabia ambayo huathiri kisaikolojia na ni hatari kwa afya.

Ifuatavyo ni njia ya kisaikolojia ambayo mwanamke anaweza kutumia kumpata mwanaume mwenye kumfaa bila kufanya naye mapenzi tena ni jibu sahihi la kuondokana na mchezo wa kubahatisha kwa wanaume wanaosaka wapenzi wa kweli na si taksi bubu ambazo mchana huweka namba za njano usiku nyeusi.

KWANZA- Ni ya mwanamke/mwanaume mwenyewe kujifahamu na kufahamu vigezo vya mpenzi anayemhitaji katika maisha yake. Ifahamike kuwa kila mwanaume ana wake na kila mwanamke anaye wake wa maisha pia. Hivyo asiyekufaa wewe anawafaa wengine, kinachotakiwa ni wewe kujitambua kwanza ili umtambue umtakaye.

Wanawake/wanaume wengi hawafahamu wanahitaji wapenzi wa aina gani, hivyo wanajikuta kama watu wanaoingia sokoni bila kujua wanataka kununua nini? Ndiyo maana wengi wameangukia kwa matapeli wa mapenzi, wakachezewe na kuumizwa moyo bure.

PILI- Ni kuketi chini na kuorodhesha vigezo stahili vya mwanaume/mwanamke unayemtaka. Baada ya hapo orodhesha tena kasoro za mwanaume/mwanamke unazoweza kuzivumilia na zile ambazo huwezi kuzivumilia kabisa. Hii inatokana na ukweli kwamba mwanadamu hajakamilika, ana upungufu wake.

TATU- Anza kumsaka kwa kutumia milango ya fahamu. Cha kufanya hapa ni kuruhusu macho yawaone wanaume/wanawake na kuwatathmini kwa maumbile yao ya nje na kisha kupata majibu kutoka moyoni juu ya kuvutia kwao ambako hutambulika kwa moyo kurithika na mwili kusisimka.

NNE - Kuanzisha safari ya kuchunguza tabia za nje na za ndani kivitendo. Hapa suala la ukaribu baina ya mwanaume na mwanamke linahitajika. Msingi unaotajwa hapa ni kujenga mazoea ya kawaida yasiyokuwa na masuala ya kimapenzi na ngono. Kutambuana, dini, viwango vya elimu, kabila na makundi ya marafiki ni mambo ya kuzingatia.

Katika uchunguzi huu mwanamke/mwanaume anayetafuta mpenzi hana budi kupitia na kumlinganisha huyo aliyempata na vigezo alivyojiwekea. Zoezi hili liendane na kuweka alama ya pata kila anapobaini kuwa mwanaume/mwanamke anayemchunguza amepata moja ya vigezo vyake. Lakini pia aweke alama ya kosa kwa kila kasoro anayoivumilia na ile asiyoivumilia.


 TANO - Ajipe muda wa kutosha kati ya miezi sita na mwaka kumchunguza huyo mwanaume, kisha aketi chini na aanze kujumlisha alama za vigezo alivyovijiwekea na jinsi mwanaume huyo alivyopata au kukosa.

Ikibainika mwanaume aliyechaguliwa amepata zaidi ya nusu ya alama ya vigezo vilivyowekwa, basi ujue kuwa anafaa. Kuhusu alama chache alizikosa anaweza kusaidia kuzikamilisha polepole wakati wa maisha ya ndoa.

Lakini angalizo kubwa kabisa ni kwamba mwanaume/mwanamke akionekana kuanguka katika kasoro zisizoweza kuvumilia kwa zaidi ya alama tatu. Yaani kwa mfano ni mlevi, mwizi, muongo, mbishi na katika hizo kashindwa 3, huyu hafai, ni vema akawekwa kando kwani huwezi kubeba kero 3 kwa pamoja katika maisha.

SITA - Kusajili mapenzi yenye malengo yanayotekelezeka. Lazima baada ya kuchunguzana kwa kina wapenzi watengeneze muongozo wa mapenzi yao. Wasiwe kama wanyama, lazima mipango ya wapi wametoka walipo na wanapokwenda.

Hata hivyo watalaam wanasema lazima wapenzi wapime umakini wao kwa vitendo. Kama wamekubaliana kuoana, suala la mume kwenda kujitambulisha kwa wakwe na hatua ya kuiendea ndoa ionekane. Usiri usiwepo tena. Kila mmoja amuone mwenzake kama sehemu ya maisha yake na mara zote wasaidiane kwa ukaribu.

SABA - Ni vema ndugu wakashirikishwa ili kuwapa nafasi na wao ya kuamua kama mapenzi hayo ni budi yakaendelea au yakasitishwa. Ni ukweli ulio wazi kwamba licha ya wengi kupuuza maamuzi ya ndugu kwa madai ya kuwa hawana nafasi kwa wapenda nao, lakini uchunguzi unaonesha kuwa wapenzi wengi huacha kutokana na sumu za ndugu hasa pale wanapokuwa wameonesha kutounga mkono uhusiano wa wanaotaka kuoana

NANE - Hatua hii ni ya kuweza kuzungumzia ufanyaji mapenzi, hapa nina maana kama wapenzi wamejizuia kwa muda mrefu na wanahisi kuchoka wanaweza kujadiliana kuhusu hilo na kuamua ufanyaji huo wa mapenzi una lengo gani, kama ni kuburudisha miili basi suala la afya na uzazi salama litazamwe.

TISA - Kutimizwa kwa ahadi ya kuoana ni hatua ya tisa ambayo nayo si busara ikachukua muda mwingi kutekelezeka, kwani ucheleweshaji mwingi wa ndoa nao huvunja moyo na mara nyingine umewafanya wengi kutoaminiana.


 KUMI - Kuamua kuwa mwili mmoja kwa kuvumilia na kuwa tayari kukabiliana na changamoto zote za maisha ukiwemo mkwamo na dhiki ambazo huchangia sana ndoa nyingi kuvunjika. Hapa pia ni wajibu wa wanandoa kuchukuliana udhaifu na kusaidia, kuwa tayari kujifunza na kujali zaidi upendo kuliko hisia za mwili ambazo wakati mwingine hudanganya na hivyo kumfanya mwanandoa asivutiwe na mwenzake.

Mwisho ni kwamba kanuni hizi huwafaa watu wazima mapenzi ya kitoto hayawezi kujenga misingi hii imara mara nyingi ni kudanganyana, kuharibiana maisha, kupeana mimba na maradhi

Thursday 21 April 2016

DARASA LA CHUMBANI


      

CHENI ZA KIUNONI WAKATI WA

                TENDO LA NDOA



Uvaaji wa cheni au shanga kiononi kwa wanawake ni aina ya utamaduni ambao umekuwa ukipendwa sana na wanawake hasa wa pwani tangu miongo mingi iliyopita na kutokana na mabadiliko ya ya kiutamaduni na kuenea kwa utandawazi wanawake wengi wamekuwa wakivaa shanga au cheni kiunoni kama fasheni tu au urembo pasipo kujua matumizi, Loo!

Vile vile kwa upande wa wanaume nao wamekuwa sio wataalamu katika kuzitumia shanga/cheni hizi ziwapo kiunoni mwa wapenzi wao na hivyo kupunguza ari ya wao kufaidi tendo lenye raha kuliko matendo yote,namaanisha kutiana.

Zifuatazo ni baadhi tu ya namna ambavyo shanga au cheni za kiunoni huweza kuleta kizaa zaa kwa mwanaume na hata mwanamke mwenyewe na kumfanya asisimke kimahaba jambo linalotia ashki sana pale mnapojiandaa kula lile tunda taam ambalo hata chokleti haifikii.

*Kitendo cha mkaka kuona cheni/shanga kadhaa zimetokeza tu kiunoni mwa mdada mrembo ambaye anavutia na kujitunza basi ni mistake tosha mkaka huyo amefanya kwa kuchungulia chungulia kwenye viuno vya watu wenye taaluma zao.

Cheni/shanga hizi huleta muonekano mzuri sana pale zinapokuwa zimefanya mizunguko kadhaa kiunoni mwa mdada ambaye anajithamini na kujijali hivyo mwanamume aliyetimia lazima asisimke na kujawa na hisia za matamanio ya hali ya juu kwa kuona shanga/cheni hizo na kama kwa bahati nzuri mdada ukamfuma mkaka huyo akiangalia kiunoni hapo utamuana jinsi alivyozuzuka na macho ya uchu yamemtoka kwa kuona vifaa nyeti vya kumkolezea mwanaume chumbani.

*Cheni/shanga hizi hutumika kuchezewa kwa ustadi na wanaume waliobobea katika haya majamboz hasa pale wanapotumia ndimi zao kuzungusha kiunoni mwa wapenzi wao huku shanga/cheni hiyo ikiwa mdomoni na ulimi ukitumika ipasavyo katika kugusa na kutekenya ngozi ya mpenzwake na mazingira yote ya jirani ilipopita shanga hizo kama vile kwenye kinena,na hata kumani. Mtekenyo huu ukifanywa kwa ustadi hakika mwanamke hujihisi burudani sana kifaa chake hicho cha kiunoni kilivyopata mtumiaji.

*Shanga/cheni hutumika katika kuamsha uume pale unapoonekana kuanza kulala. Kwa kutumia cheni wanawake wataalam huchukua uume wa mpenz wake na kuupenyeza au kuuviringisha juu ya shanga/cheni hiyo mithili ya mtu anayesukuma chapatti hivyo hufanya uume wa mtu wake kupata nguvu na amsha amsha ndani ya muda mfupi na hivyo iwapo tayari imesimama huingizwa taratibu kumani tayari kufanya shughuli yake ya kukuna sehemu husika mpaka pale mwanamke anapokiri kweli hakuna raha kama kutiwa pale unapompata mtiaji
 DARASA LA CHUMBANI
 NINI KAZI YA 'SHANGA ZA KIUNONI, KITANDANI
 NA NINI MAANA YA RANGI ZAKE.
,naomba tuongelee rangi za shanga kwa wale wanaopenda kuvaa shanga.
Najua wengi mtakuwa mnafahamu rangi na maana zake lakini kwa wale wasiojuwa amawanaopenda kuvaa lakini wanajinunulia rangi yeyote huu ndo wakati mwafaka.
Wanaume wengi wanaopenda wanawakewao wavae shanga ili kusisimuana tu .Je mnafahamu zinamaanisha nini?. ...Karibu tujifunze pamoja.
Katika swala la mahaba shanga hutumika kusisimuana haswa pale utakapompata mwanaume anayejuwa kuzitumia vizuri na unaweza kuvaa hata kumi ukitaka . Jana niliguswa sana na simulizi la rafiki yangu juu ya shanga, hivyo nikaona boraniandike na wengne wajue.Hii ni sehem ndgo ya simulizi lake.
".........Nilikutana na boyfiriend wangu maeneo ya Shycom …tukaelekea kwenye disko. Tulikuwa tunacheza madensi, halafublues, ya Boyz to Men ikaanza kupigwa. Wenye disko walipunguza taa. Mimi na boyfriend wangu tukakumbatiana na kuanza kucheza Blues.
Miili yetu iligusana na akaana kunipapasa taratibu kufuatana na beats za muziki. Nilifurahi sana. Akateremsha mikono yake kwenye kiuno changu.
Alivyogusa shanga zangu akawa kama mwili wake umekufa ganzi. Alisisimuka we! Akanishika kwa nguvu, niligundua kuwa ham yake ilikuwa juu....."
Naamini utakuwa umejifunza kitu fulani muhimu kutokana na simulizi hilo.Sasa turudi kwenye mada yetu.
Kuna wengine wanananunua rangi kama pink, blue, gold hizi rangi hazina maana kwenye sita kwa sita ni urembo tu kupendezesha kiuno.

RANGI ZENYE MAANA PINDI UWAPO 
KITANDANI NA MPENZI WAKO

Nyekundu :

ukimkuta mwanamke amevaa shanga ya rangi hii unatakiwa kuelewa kwamba mwanamke huyu yupo kwenye hedhi, kwahiyo wewe fanya mengine lakini sio kutumbukia unless yeye mwenyewe amekuruhusu na wewe uwe na uwezo wa kutumbukia hata akiwa kwenye hedhi (kitu ambacho kiafya akishauriwi).

Nyeupe:

ukimkuta mwanamke amevaa shanga nyeupe hii humaanisha hana tatizo lolote litakalomfanya asikupe raha ya sita kwa sita, kwahiyo ukitaka tu muda wowote unapata.

Nyeusi:
 ukimkuta mwanamke amevaa rangi nyeusi hii humaanisha ya kwamba yupo tayari kukupa raha za sita kwa sita lakini uwanja wake haujakatwa majani, kwa hiyo chaguo ni lako kama unataka kutumia siku nzima kutafuta goli haya, ama kama utamsaidia kumkatia majani uwanjani vizuri zaidi ama kama huwezi yote basi mpe muda akate mwenyewe. 
karibu kujifunza zaidi
 Call +255 779 528 779
        +255 676 747 784

Wednesday 20 April 2016

MAHUSIANO

 MFANYE MWANDANI WAKO

 ATABASAM KWA 

KILA MESSEGE NZUURI 

YA MAPENZI UTAKAYO MTUMIA 

NAZO ZIKO HAPA.. 

Mahusiano Kwanza
+255 779 528 779
+255 676 747 784
 

 ahaba unayonipa natamani niwe
nawe mpaka
kufa,
kila siku zinavyozidi kupita
najuta kwanini nilichelewa penzi
kukupa,
nakupenda na nitakupenda hadi
kufa!
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Hivi ni lini penzi utanipa,
nimechoka na ahadi
unazonipa kila kunapokucha,
tambua kwako nimefika na siku
utakayonipa
zawadi nzuri nitakupa na
hutanisahau
hadi kufa.
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Nisamehe la azizi ukweli mbona
uko wazi,
yule si wangu mpenzi ila ni rafiki
yangu
kipenzi, yangu mapenzi ni wewe
pekee nayekupa mpenzi,
katika hii dunia ni wewe
pekee penzi nayekupatia!
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Uko wapi wangu malkia, mwenzio
hamu nasikia nawe
ndiye ujuwaye hamu kunitoa,
tafadhali dear upatapo msg hii
tambua nyumbani
nakusubiria! Luv u
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Hakika raha wajua kunipatia,
fimbo wajua kuitumia sharti
mtoto wakike nabaki
nagugumia kwa raha unayonipatia
ambayo wengi
wanaililia , plz utamu wangu
nitunzie!
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Nashukuru kwa miguno
uliyonipatia na kiuno kunikatia,
utamu niliousikia
nilitamani kulia hatima
ilipowadia , nakupenda
dia usije utamu wangu mwingine
kumpatia! Luv u
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Wikiendi ndiyo imeisha,
majukumu hatunabudi kuyatimiza
dear,
kuwa nawe muda mrefu
nimefurahia nakujihisi malkia
katika hii dunia kuwa
nawe najivunia. Luv u
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Wangu Malkia nashukuru kwa
mahaba uliyonipatia,
nikikumbuka miguno na viuno
ulivyonipatia na
raha niliyojisikia, nahisi kuna
mwingine unampatia,
please dear penzi langu usije
wengine kuwapatia! Nakupenda.
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Nashukuru kwa yako dozi hakika
katika
mapenzi wewe ni mkufunzi,
wajua bakora kuitumia, mpenzi
usije ukawa na
mwingine
unayempatia, hakika nikijua
nitaumia kama
sikujiuam. Nnakupenda!
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Nimeamini wewew ni mtalam
wajua kunitoa hamu,
unipapasapo huhisi kupoteza
fahamu, maneno yako
matamu hunizidisha hamu, hakika
wajua kunikamua, luv u.
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Hakika nimepata tabibu, maradhi
yangu wajua
kujyatibu,
napenda jinsi unavyonitibu,
huna papara yaani ni taratibu,
mpenzi usijemuonyesha
mwingine hizo
zako zabibu,
maswahibu yakatayonisibu hakuna
atakayeweza kuyatibu, nakupenda.
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Usiku wa jana ulikuwa wa aina
yake, ulinipa mambo
matamu yasiyo ya kawaida,
ulinifurahisha sana mpenzi
wangu,
ulidhihirisha kuwa wewe ni
kidume
uliyeubwa kwa ajili yangu..
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Nakumbuka siku utamu ulityonipa
maneno
matamu kedekede hukusita
kunipa na
ahadi kibao masikioni mwangu
zilisikika,
hakika roho yangu haikusita
kuamini
kwako nimefika, nashangaa
leo utamu hutaki nipa!
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Wikiend ndiyo siku niliyokuwa
nikiisubiria mimi
nawe mpenzi tupate tulia,
mahaba na
maneno matamu ndio zawadi
niliyokuandalia. Kumbuka yetu
miadi na jali wakati!
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Masika ndiyo hiyo imewadia,
baridi nalo ndio
limenichachia, mpenzi
lini waja joto kunipatia?
Mwezio naumia!
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Nashukuru kwa yako dozi hakika
katika mapenzi
wewe ni mkufunzi, wajua bakora
kuitumia,
mpenzi usije ukawa na mwingine
unayempatia, hakika nikijua
nitaumia
kama sikujiuam. Nnakupenda!
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Nimeamini wewew ni mtalam
wajua kunitoa hamu,
unipapasapo huhisi kupoteza
fahamu,
maneno yako matamu hunizidisha
hamu, hakika wajua kunikamua,
luv u.
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
Kuwa nawe najivunia, mtoto
mapenzi wayajua,
kiuno, sauti yako tamu mithili ya
chiriki wajua hasa kuitumia, mua
wangu
wajua kuukamua, ukiniacha jua
nitaumia,
nakupenda usije niacha nitajiua!
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
usiku unapoingia najawa na furaha
unajua kwanini?
unaponigusa nahisi tumeumbwa
wawili,
mchana nakumisi sana unapokuwa
kazini,
wikiendi natamani isiishe kwani
unanipa
raha ambazo siwezi kuzipata
popote. . .
Naomba raha hizi usimpe
mwingine. . .
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
kila ninapoona macho yako
nafurahia uwepo
wako,nikiona tabasamu
lako,nasikia homa ya
moyo,nikiona chozi lako la furaha
,moyo wangu unakuwa
huru kwako,nakupenda sana
mpenzi
wangu na
wewe ndiye valentine wangu. . .
Pokea busu mwaaaah
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
pumzi yako kwangu ni burudani ya
ajabu,
nakupenda sana busu lako
maridhawa
shavuni mwangu.wewe ndiye
furaha
yangu



Saturday 16 April 2016

DALILI 20 ZA MWANAMKE ASIYEKUPENDA KWA DHATI!

  1. DALILI 20 ZA MWANAMKE ASIYEKUPENDA 

    KWA DHATI!

     

    Mpenzi msomaji/mfatiliaji wa blogg hii ya Mahusiano Kwanza. 

    leo ningependa niwafahamishe kuhusu hili...  

     Dalili 20 za mwanamke

     asiyekupenda kwa dhati! nazo ni...

    1. 1 : Hataki kuambata na wewe katika matembezi na ikitokea anakuwa mtu wa masharti mara akuambie tangulia nakuja au pengine kutembea nawe kwa umbali.
      2 : Anapata kigugumizi kukutambulisha kwa rafiki zake na ndugu na inapotokea amebanwa hafikishi ujumbe kwa kiwango timilifu.
      3 : Haoneshi kubana matumizi kwa ajili ya maendeleao, kwake ni kufuja mali na anapokosa kupewa pesa ni mwepesi kulalamika na wakati mwingine kununa kabisa.
      4 : Anaahilisha mara kwa mara kukutana na wewe tena bila kukueleza sababu za msingi Au kukutungia uongo wa dhahili na kuusisitiza bila kuona aibu.
      5 : Anapokuwa akitoa maelezo ya mwanaume amtakaye sifa zake zinakuwa hayalingani na wewe. Anaweza kukuambia napenda kuishi na mwanaume mwenye gari au mwenye mwili mkubwa, sifa ambazo wewe huna!
      6 : Hacheki kwa furaha hata kama ukimchekesha haoneshi furaha ya moyoni. Tena mara nyingine anakuwa mkimya na mshiwishi mkubwa wa kuachana kutoka kwenye matembezi yenu ya jioni. “Aaah, mi nimechoka narudi nyumbani”
      7 : Anajaribu kukuunganisha na wanawake wengine na haoni vibaya anaposikia unamfukuzia mwingine badala yake anakutia moyo wa kuendelea na usaliti wako. Hana wivu kabisa.
      8 : Hajuti anapokukosea, mwepesi wa kujitenga, kutokuzungumza nawe na mwingi wa kukusukumia makosa hata kama yeye ndiye aliyekukosea.
      9 : Msambazaji wa habari za udhaifu wako na mtu asiyekusifia mbele za wenzake. Si balozi mwema kwa familia yake, haishi kukuponda mbele ya wazazi na ndugu zake.
      10 : Mwepesi wa kupokea na si wa kutoa mmiliki wa mali zako na mkumbatiaji wa mali zake pia. Msiri wa mipango yake na mtu anayependa kujua zaidi ya kwako kuliko wewe kujua yake.


  1. 11: Hathamini uwepo wako na anakuchukulia kama mtu wa akiba. Hakumis unapokuwa haupo,
  2. hahisi upweke wala hakukumbuki unapokuwa mbali naye.
  3. 12 : Hakutii moyo unaposhindwa na mara nyingine hauzuniki nawe unapokuwa una shida,. Hachukui huzuni yako kama yake, hakufariji na hakusaidii kutatua kilichokwama.
  4. 13 : Mhamasishaji wa uasi hasa wa watoto na ndugu, anayeweza kuchochea hisia za jamii ikuone mbaya, ukudharau na wakati mwingine ikutenge. Mwenezaji wa sifa zako mbaya.
  5. 14 : Hakupi kipaumbele katika maamuzi, anajiona yeye ndiye wa kwanza na wewe ni mtu wa kufuata hata unapopinga hasitishi dhamira yake ya kutenda.
  6. 15 : Humsisimui katika mambo ya faragha, anakuchukulia kama ndugu yake.

 

16 : Hakuhudumii tendo la ndoa mpaka siku amependa mwenyewe. Ni mwingi wa sababu za kuchoka kusingizia ugonjwa na mwenye kuhisi kero ya kucheza nawe mchezo wa kikubwa.

  1. 17 : Hazungumzii maendeleo yenu, mwepesi wa kushawishi ilivyopatikana viuzwe ili atimize hitaji lake. “Niuze simu yangu niende kuwaona wazazi, maana kuna sherehe ya motto huko!”
  2. 18 : Hataki kuambiwa ukweli na anapotokea akaambiwa anajitetea kwa kumtaja mwanaume mwingine. “Mbona Shabani (si jina halisi) anamfanyia hili, hamfanyii hivi mkewe”
  3. 19 : Hasamehe na kusahau. Kosa la mwaka juzi analijengea hoja.
  4. 20 : Mwepesi wa kutoa kauli za kutengana na asiyeogopa kuachwa. “Kama vipi kila mtu akae kivyake maana naona unaniboa tu, unadhani nitashindwa kuishi bila wewe”

kwa maoni/ushauri zaid tuwasiliane hapa

+255 779 528 779

+255 676 747 784

 

Thursday 14 April 2016

KARIBU

Mahusiano Kwanza: Habari wapenzi wa blog hii mpya ya Mahusiano Kwanz...: Habari wapenzi wa blog hii mpya ya Mahusiano Kwanza . Karibuni tujumuike pamoja na tupeane mawazo ktk kila habari tutakayopeana humu. Na...